Header Ads

TIBA ASILIA YA MAFUA

TIBA ASILIA YA MAFUA

Kuna mafua ambayo wakati mwingine hutokea au kikohozi kwa ajili ya hali flani ‘seoson’. Tiba ya ugonjwa huu ni:
Bizari-Turmeric
Weka bizari kwenye kila mlo wako kwa ajili ya kinga kwani mbali na kutibu inasaidia pia kukinga.
Mdalasini –Cinnamon
Tumia chai ya mdalasini kila unapojisikia kiu, ni tiba tosha kwa mafua au kikohozi hicho cha wakati.
Asali-Honey
Tumia kijiko cha asali kila siku, unaweza kufanya hivyo kwa kuweka kwenye maji ya uvuguvugu.
Unga wa kitunguu swaumu au kitunguu maji
Chukua unga wa vitunguu hivi, changanya na unga wa tangawizi kisha weka kwenye unga wa ‘mastard’. Ukishapata mchanganyiko huu, koroga kisha kunywa kwa siku mara tatu, utapona kabisa tatizo lako.
LimaoKamua limao kwenye maji ya uvuguvugu, kunywa kila siku mpaka kipindi hicho kitakapoisha.
Chumvi
Chukua ¼ ya kijiko cha chumvi, hakikisha chumvi hiyo ni aina ayodini, changanya chumvi kwenye bilauri yenye maji kisha koroga mpaka chumvi itakapoyeyuka.
Ukishamaliza unaweza kuweka kwenye chupa ambayo unaweza kudondoshea puani, hii ni tiba nzuri kwa mafua.

No comments:

Powered by Blogger.