Header Ads

Ishara za Kupata Mtoto wa Kike Wakati wa Ujauzito


Ukitambua kuongezeka kwa mapigo ya moyo,mpaka 140 -160 kwa dakika inaweza kuonyesha kuwa unatarajia mtoto wa kike.
Magonjwa ya asubuhi
Wakati unatarajia mtoto dalili za mwanzo ni kupata magonjwa ya asubuhi, na kichefchefu ni moja kati ya ishara za kupata mtoto wa kike.
Kutokwa chunusi ghafla
Kutokwa na chunusi wakati wa ujauzito ni moja ya ishara za kupata mtotot wa kike.
Nafasi na mkao wa tumbo
Mkao wa tumbo ni ishara moja ambayo inaweza kufanya ugundue  jinsia ya mtoto. Kama tumbo lipo kwa juu au katikati inaonyesha kuwa utapata mtoto wa kike.
Mabadiliko ya tabia
Jinsia ya mtoto ambae hajazaliwa huchangia sana mabadiliko ya tabia ya mama. Wamama wenye hasira sana na wababe huonyesha kuna matarajio ya kupata mtoto wa kike.
Ukubwa wa matiti
Wakati wa ujauzito, matiti huongezeka na kuwa makubwa wakati ukijiandaa kunyonyesha mtoto wako mtarajiwa, kama una ujauzito wa mtoto wa kike titi lako la kushoto linakuwa kubwa kuliko lile la kulia.
Kipimo cha kitunguu saumu
Unapokula kitunguu saumu na harufu yako kubaki kama ile ya kawaida basi unatarajia kupata mtoto wa kike. Ukiwa unatarajia mtoto wa kiume ukila kitunguu saumu harufu hupenyeza kwenye ngozi yako na kubaki mwilini mwako.
Namna ya kulala
Wakati wa ujauzito unahisi uchovu haraka sana,na nyakati hizo ukilala sana ubavu wa kulia inamaanisha utapata mtoto wa kike.
Utafiti wa umbo la kichwa
Kama unatarajia mtoto wa kike, katika kipimo cha “ultrasound” kitaonyesha muundo wa kichwa na taya ya chini kuwa duara kama unatarajia mtoto wa kike.
Kipimo cha baking powder
Chukua baking powder kijiko kimoja changanya na maji kwenye glasi alafu changanya na mkojo wako kidogo, kama utabadilika na kuwa mzito kwa mbali, basi unatarajia mtoto wa kiume lakini baada ya kuchanganya mkojo na mchanganyiko wa baking powder na maji, na hakuna mabadiliko yoyote basi unatarajia mtoto wa kike.
Ulaini wa nywele na mng’ao
Kama nywele zako ni nyembamba na kukatika inamaanisha unatarajia mtoto wa kike, hata hivyo nywele zinazong’aa na kuvutia ni ishara ya kwamba unatarajia mtoto wa kiume.
Rangi ya mkojo
Rangi ya mkojo wako husaidia sana kuweza kutambua jinsia ya mtoto wako, rangi ya njano ya mkojo huashiria sana kwamba unapata mtoto wa kike.
Kutamani kula vitu vitamu
Kutamani kula vitu vitamu kama pipi, chocolate,ice cream ni ishara unatarajia kupata mtoto wa kike. Kutamani vitu vya chumvichumvi ni ishara kuwa unatarajia mtoto wa kiume.
Matiti kuongezeka ghafla
Utatambua kuongezeka ghafla kwa matiti hii ni ishara mojawapo kwamba unatarajia kupata mtoto wa kike. Katika kipindi hiki kama ni mtoto wa kiume mabadiliko hata hayataonekana.
Kuwa mkarimu.
Inasemekana kuwa mkarimu kipindi chote cha ujauzito ni ishara kwamba unatarajia kupata mtoto wa kike.

No comments:

Powered by Blogger.