Header Ads

Vidokezo vya Urembo Kipindi cha Ujauzito


Ni vipi nitaonekana mrembo kipindi cha ujauzito ni swali wanalokuja nalo wakina mama wengi. Kuna njia kumi sahihi za kukusaidia kufurahia urembo wako hasa katika kipindi maalumu maishani mwako.
  1. Kunywa maji
Kipindi cha ujauzito unahitajika kupata maji mengi kwa siku. Yatakusaidia kusafisha na kutoa taka na sumu mwilini mwako. Zaidi maji yanasaidia kutunza kiasi cha kimiminika kinachotakiwa mwilini mwako. Maji ni muhimu zaidi kwa afya yako na mwanao. Kunywa angalau lita 2 za maji kwa siku.
  1. Mlo sahihi
Unahitaji uangalizi na umakini wa ziada katika chakula unachokula wakati wa ujauzito na afya yako. Inashauriwa kumuhusisha daktari wako kukuandalia ratiba ya aina ya chakula unachotakiwa kula. Fuatilia ratiba hii kwa umakini, kula kwa afya, ikiwa pia ni muhimu kwa ajili ya mtoto wako.
  1. Pata muda wa kulala
Uchovu ni dalili moja wapo anazopata mama mjamzito hasa katika kipindi cha mwanzo. Kupumzika vizuri ni muhimu kwa ajili ya mwili na akili yako mwenyewe. Hakikisha unapata muda mzuri na wa kutosha kupumzika kiasi kwamba mwili wako uwe unahisi uchovu kidogo. Jiweke huru wakati wa kulala. Pumzika kwa usahihi, unaweza kutaka kutumia mito au kitu kingine cha kukuweka huru unapolala.
  1. Uzito sahihi
Unahitajika kuangalia uzito wako kipindi cha ujauzito. Baadhi ya wakina mama wanakula chochote na kila kitu pasipo kuhofia kuhusu uzito. Ikiwa ni kawaida kuongezeka uzito wakati wa ujauzito, si vema kiafya kuongezeka katika njia tofauti. Uzito unaongezeka kwa kula vyakula ambavyo havina msaada mwilini, mara kwa mara kula mlo sahihi, unaweza kumuhusisha daktari wako kwa machaguo bora.
  1. Mazoezi
Ndio, ni muhimu! Kuna mazoezi maalumu kwa ajili ya wajawazito. Hudhuria darasa la mazoezi ya yoga yaliyoandaliwa kwa ajili ya wajawazito, pata muda wa kukutana na wajawazito wengine na kujifunza na kupata uzoefu. Unaweza pia kumuomba ushauri daktari ni michezo gani unaweza kushiriki.
  1. Epuka michirizi
Wakina mama wengi wanalalamika kupata michirizi baada ya kujifungua. Unahitaji kuchukulia uangalizi hili wakati wa ujauzito.  Tumia cream uliyoshauriwa au zinazouzwa kwa ajili ya kuondoa michirizi. Tumia kila siku kuukanda mwili wako. Unaweza pia kutaka kuepuka kukimbia, kuruka au kugonga kama njia ya kuepuka michirizi.
  1. Thamini umbo lako
Pindi unatoka katika matembezi vaa nguo ya kuonyesha umbo lako, umbo la mwanamke ni zuri wakati wa ujauzito, ujauzito unamuongezea hipsi mwanamke. Tumia nafasi hii kuvaa nguo za kushika mwili wako vizuri ili kuonyesha vema hipsi zako.
  1. Uangalizi wa ngozi
Pamoja na yote wakati wa ujauzito, usisahau ngozi yako. Urembo katika kipindi cha ujauzito ikiwemo urembo wa ngozi, kwa kupendelea mimea tiba katika kipindi sahihi. Kutokana na mabadiliko ya homoni kunaweza kuwa na athari kidogo katika ngozi yako. Unaeza kutumia bidhaa za kulinda ngozi kwa kuzingatia aina ya ngozi yako lakini hakikisha hutumii kemikali hatarishi.
  1. Make-Up
Mwanamke hachukizwi na make up! kutokana na mabadiliko ya homoni unaweza kupata madoa usoni hivyo poda ni mkombozi. Make up ndio mkombozi, tena angalia zile ambazo hazitumii kemikali kali.
  1. Pumzika
Mwisho na muhimu zaidi ni kukumbuka kupumzika, weka mapumziko katika ratiba yako. Lala chini kwa muda unapopata nafasi. Pumzisha mwili wako. Ujauzito unaweza kuja na stress sana lakini hakikisha hazikushindi, jinsi unavozidi kupumzika ndivo jinsi unaonekana mrembo.

No comments:

Powered by Blogger.